KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 17, 2011

Rose, Bahati wapigwa kumbo


WANAMUZIKI nyota wa Injili nchini, Rose Muhando, Bahati Bukuku na Flora Mbasha mwishoni mwa wiki iliyopita walishindwa kung’ara katika tuzo za muziki huo baada ya kupigwa kumbo na waimbaji chipukizi.
Licha ya majina ya waimbaji hao watatu kuwemo katika tuzo ya mwimbaji bora wa kike, walifunikwa na waimbaji chipukizi Martha Mwaipaja, Christina Shusho, Upendo Nkone na Upendo Kilahiro.
Mshindi wa tuzo hiyo alikuwa Christina, ambaye aliwafunika vibaya Rose na Bahati.
Boniface Mwaitege aliibuka mshindi wa tuzo ya mwimbaji bora wa kiume wakati tuzo ya kundi bora la mwaka ilinyakuliwa na Double E.
Tuzo ya wimbo bora ilinyakuliwa na mwimbaji mkongwe Upendo Nkone wakati tuzo ya video bora ya mwaka ilinyakuliwa na John Lisu kupitia wimbo wake wa Jehova yu hai.
Mwimbaji chipukizi Miriam Shilwa alitwaa tuzo ya balozi bora wa jamii baada ya kumshinda Flora.
Mratibu wa tuzo hizo kutoka Tanzania Gospel Music Award (TGMA), Harris Kapiga alisema washindi walipatikana kutokana na kupigiwa kura na mashabiki wa muziki huo.
Wanamuziki wengine wa kiume waliopigiwa kura ya kuwania tuzo ya mwimbaji bora wa kiume walikuwa Jackson Bent, Fanuel Sedekia, Ambwene Mwasongwe na John Lisu.
Waimbaji wengine waliokuwa wakiwania tuzo ya wimbo bora ni Christina Mbilinyi ‘Nasubiri baraka zangu’, Miriam Mauki ‘Double Double’, Upendo Kilahiro ‘Usifurahi mwenzako anapofanikiwa’ na Martha Mwaipaja ‘Usikate Tamaa’.
Tuzo ya wimbo bora kwa wanaume iliwaniwa na Thomas Bernard ‘Jehova ananipa kushinda’, Christopher Israel ‘Hosana’, Danford Sunday ‘Mwacheni Mungu’, Aaron Kyara ‘Juu Mbinguni’ na Charles Thobias ‘Akili zangu zimefika mwisho’.

No comments:

Post a Comment