KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, March 4, 2011

Acheni kunifuatafuata


MWIGIZAJI filamu nyota wa Nigeria, Stella Damasus amewataka watu waache kufuatilia maisha yake binafsi, badala yake wajikite zaidi katika kazi yake.
Stella alisema mwishoni mwa wiki iliyopita mjini hapa kuwa, uhusiano wake na watu ni kazi anayoifanya na siyo kile kinachotokea chumbani kwake.
“Watu wanapaswa kujifunza kuacha kufuatilia maisha yangu. Chochote kinachohusu maisha yangu nje ya kazi, sipendi kukizungumzia,”alisema mwigizaji huyo ambaye pia anamiliki bendi ya muziki.
Stella pia aliwashushia lawama nzito waandishi wa habari wa Nigeria kwa madai kuwa, ni wachache sana wanaoandika habari za uchunguzi. Alisema wengi wamekuwa wakiandika habari za uzushi na uchochezi.
Mcheza filamu huyo alisema anapenda kuishi maisha ya kawaida na hataki kuona umaarufu wake ukiathiri maisha yake kwa namna yoyote.

No comments:

Post a Comment