KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, March 4, 2011

Samatta aipania Yanga


Na Aboud Mahmoud, Zanzibar
MSHAMBULIAJI Mbwana Samatta wa Simba amesema amejigamba kuwa, lazima awafunge mabao mahasimu wao Yanga katika mechi kati yao keshokutwa.
Akizungumza na Burudani mjini hapa juzi, Samatta alisema amejipanga vyema kuhakikisha anaifunga Yanga kwa mara ya kwanza akiwa amevaa uzi wa Simba.
Samatta alisema anaridhishwa na mazoezi wanayopewa na Kocha wao Patrick Phiri kwa ajili ya mechi hiyo na kusisitiza kuwa, wamejipanga vyema kulipa kisasi cha kufungwa na Yanga katika mzunguko wa kwanza.
Mbali na kushinda mechi hiyo, Samatta alisema lengo la timu yake ni kutwaa tena ubingwa wa ligi hiyi ili wapate nafasi nyingine ya kushiriki michuano ya kimataifa.
"Nawawaomba mashabiki wa Simba wasiwe na wasiwasi na timu yao kwani mazoezi tunayoyafanya ni mazuri na pia waweke matumaini makubwa ya kuondoka na ubingwa,”alisema.
Mshambuliaji huyo aliyepachikwa jina la Golden Boy Junior, alitamba pia kuwa, hawana wasiwasi na pambano lao la michuano ya klabu bingwa Afrika dhidi ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Simba inatarajiwa kurejea Dar es Salaam kesho kwa ajili ya pambano lao dhidi ya Yanga litakalofanyika keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment