KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, June 25, 2010

SIKINDE KUTAMBULISHA MBILI MPYA

KIONGOZI wa bendi ya Mlimani Park Orchestra, Habibu Abbas Jeff akimkabidhi zawadi Amina Michael baada ya kuibuka mshindi wa kucheza miondoko ya Sikinde. Shindano hilo lilifanyika kwenye ukumbi wa DDC Kariakoo, Dar es Salaam.
MASHABIKI wa Mlimani Park Orchestra wakijimwayamwaya kwenye ukumbi wa DDC Kariakoo, Dar es Salaam.

WAPULIZA Tarumbeta, Mbaraka Othman (kushoto) na Hamisi Milambo wakifanya vitu vyao.


WAIMBAJI Abdalla Hemba (kushoto) na Hassan Bitchuka wa Mlimani Park Orchestra wakiwajibika jukwaani.

BENDI ya muziki wa dansi ya Mlimani Park Orchestra ‘Sikinde’ imeibuka na vibao viwili vipya, vinavyotarajiwa kutambulishwa rasmi kwa mashabiki mwishoni mwa wiki hii.
Msemaji Msaidizi wa bendi hiyo, Emmanuel Ndege alisema mjini Dar es Salaam juzi kuwa, vibao hivyo vimetungwa na mwimbaji mkongwe, Shaaban Dede.
Alivitaja vibao hivyo kuwa ni ‘Mapenzi kitu cha ajabu’ na ‘Mwanamke kumwezesha’.
Kwa mujibu wa Ndege, vibao hivyo vitapigwa kwa mara ya kwanza katika onyesho litakalofanyika Jumapili kwenye ukumbi wa DDC, Kariakoo, Dar es Salaam.
Alisema kutungwa kwa vibao hivyo ni maandalizi ya utambulisho wa albamu mpya ya bendi hiyo, inayotarajiwa kukamilika hivi karibuni.
Mbali na kutambulisha vibao hivyo, Ndege alisema bendi hiyo imeanzisha utaratibu wa kuwapa zawadi mashabiki wake kupitia mashindano ya kucheza miondoko ya Sikinde na kuimba.
“Kuanzia wiki iliyopita, tulianzisha shindano la kucheza miondoko ya Sikinde na washindi wawili wa kwanza walipata zawadi zilizotolewa na wanachama wetu wa kundi la Sikinde Family,”alisema.
Aliwataja washindi hao kuwa ni Amina Michael kwa upande wa wanawake na Sirikali Msumali aliyeibuka mshindi kwa wanaume. Hata hivyo, hakutaja zawadi zilizotolewa kwa washindi hao.
“Hiyo ni siri yao, tunachokifanya ni kuwakabidhi zawadi hizo pale pale ukumbini zikiwa zimefungwa kwenye mifuko maalumu. Lengo letu ni kuwashangaza na kuwaonyesha kwamba tunawapenda na kuwathamini,”alisema.





No comments:

Post a Comment