KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, June 3, 2010

Chuji, Tegete, Kigi kuondoka Yanga

WACHEZAJI watatu nyota wa klabu ya Yanga wamepata nafasi ya kwenda kucheza soka ya kulipwa nje ya nchi.
Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alithibitisha jana kuhitajiwa kwa wachezaji hao nchini Sweden na Afrika Kusini.
Aliwataja wachezaji hao kuwa ni kiungo Athumani Iddi ‘Chuji’ na washambuliaji Jerryson Tegete na Kigi Makasi.
Kwa mujibu wa Mwalusako, Tegete na Chuji wanatakiwa na klabu moja ya Sweden wakati Kigi
anatakiwa na klabu ya Afrika Kusini. Hakuzitaja klabu hizo.
Tegete aliwahi kwenda kufanya majaribio ya kucheza soka ya kulipwa katika klabu ya FK Dalkurd ya Sweden na kufuzu, lakini alishindwa kuingia nayo mkataba kutokana na kuwekewa ngumu na uongozi wa Yanga.
Katika hatua nyingine, klabu za Simba na Azam zimeanza kupigana vikumbo kumwania mshambuliaji wa timu ya mkoa wa Ilala, Marcel Kaeza.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18, aliwavutia viongozi wa klabu hizo wakati wa michuano ya Kombe la Taifa, iliyomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Dar es Salaam.
Ilala ilikuwa ikinolewa na Kocha Jamhuri Kihwelo, maarufu kwa jina la Julio, ambaye naye imedaiwa anamfanyia mipango mchezaji huyo kwenda kucheza soka ya kulipwa Qatar.

No comments:

Post a Comment