KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, June 6, 2010

Babu Chuchu afariki

ALIYEKUWA mmiliki wa bendi ya muziki wa dansi ya Chuchu Sound, Yusuf Ahmed Alley, maarufu kwa jina la ‘Babu Chuchu’ amefariki dunia.
Habari zilizopatikana mjini Dar es Salaam jana zilisema kuwa, Babu Chuchu alifia mjini Nairobi, Kenya nyakati za asubuhi, ambako alikwenda kikazi.
Kwa mujibu wa habari hizo, mwili wa marehemu ulirejeshwa Zanzibar jana na mazishi yalifanyika jana kwenye makaburi ya Mwanakwerekwe.
Hata hivyo, hakuna taarifa zilizotolewa kuhusu sababu za kifo chake, ambacho kimepokelewa kwa mshtuko mkubwa na mashabiki wa muziki nchini.
Taarifa za kifo cha Babu Chuchu zilianza kutangazwa jana asubuhi kupitia kwenye vituo mbalimbali vya radio.
Babu Chuchu atakumbukwa kwa uhodari wake katika muziki, ulioiwezesha bendi yake ya Chuchu Sound kupata umaarufu mkubwa kabla ya kusambaratika.
Umaarufu wa Babu Chuchu ulitokana na chombezo zake kwenye nyimbo za bendi hiyo, hapa alipokuwa akijibizana maneno na mwimbaji Omari Mkali.
Babu Chuchu pia alikuwa mmoja wa wajumbe wa bodi ya tamasha la kila mwaka la Sauti za Busara. Pia alikuwa akimiliki studio yake binafsi ya kurekodi muziki na kituo cha radio.

No comments:

Post a Comment