KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, May 16, 2011

Simba ikifungwa na Wydad, kuangukia Kombe la Shirikisho

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mei 16, 2011
SIMBA v WYDAD CASABLANCA
Mechi ya kutafuta nafasi ya kucheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) kuondolewa kwa kuchezesha mchezaji asiyestahili imepangwa kufanyika kati ya Mei 27, 28 na 29 mwaka huu kwenye uwanja huru (neutral ground).
Simba ya Tanzania na Wydad de Casablanca ya Morocco ndizo zitakazopambana katika mechi hiyo ya mkondo mmoja. Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) linatarajia kutaja katika muda mfupi ujao nchi ambapo mechi hiyo itachezwa.
Timu itakayoshinda itaingia katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa, ikiwa kundi B pamoja na Al Ahly ya Misri, Esperence (Tunisia) na Moloudia Club d’Alger ya Algeria.
Timu itakayoshindwa itaingia katika hatua ya 16 bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho ambapo itacheza mechi ya kwanza nyumbani na Daring Club Motema Pembe ya DRC kati ya Juni 10, 11 na 12 mwaka huu.

MAPATO STARS v BAFANA BAFANA

Pambano la kirafiki kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Afrika Kusini (Bafana Bafana) lililochezwa Mei 14 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 75,888,000 kutokana na watazamaji 10,554 walionunua tiketi.
Watazamaji 240 walilipa sh. 30,000, 585 (sh. 20,000) na 1,423 (sh. 10,000), 614 (sh. 7,000) na 7,692 (sh. 5,000).
Baada ya kuondoa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 11,576,135.59 na gharama za awali za mchezo ambazo ni sh. 21,843,600.00 mgawo ulikuwa kama ifuatavyo; asilimia 10 kwa uwanja sh. 4,246,826.44, asilimia 10 kwa gharama za mchezo sh. 4,246,826.44, asilimia 5 kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 2,123,413.22 na asilimia 75 kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 31,851,198.31.

Nacho Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kilipata asilimia tano kutoka kwa mgawo wa TFF ambayo ni sh. 1,592,559.92.

SEMINA YA WAAMUZI WA FIFA

Semina kwa waamuzi wanaotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) itafanyika Dar es Salaam kuanzia Mei 17 hadi 19 mwaka huu. Wakufunzi wa semina hiyo ni Riziki Majalla, Leslie Liunda na Omari Kasinde.

Waamuzi hao ni Ramadhan Ibada, Waziri Sheha, Oden Mbaga, Judith Gamba na Israel Mujuni. Waamuzi wasaidizi ni Hamis Chang’walu, Ally Kombo, Saada Tibabimale, Josephat Bulali, Samuel Mpenzu, Erasmo Jesse, Mwanahija Makame, John Kanyenye na Khamis Maswa.

Boniface Wambura
Ofisa Habari TFF

No comments:

Post a Comment