KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, May 15, 2011

RATIBA LIGI YA TAIFA

Ligi ya Taifa inayoshirikisha mabingwa wa mikoa itaanza Juni 11 mwaka huu katika vituo vya Sumbawanga, Kigoma, Singida na Kibaha.
Washindi watatu wa kwanza wa kila kituo watashiriki hatua ya fainali itakayofanyika katika kituo kitakachotangazwa baadaye.Kituo hicho cha fainali kitakuwa na makundi matatu ya timu nne nne.
Mshindi wa kila kundi na washindwa bora (best losers) wawili, hivyo kufanya jumla ya timu tano ndizo zitakazopanda kucheza Ligi Daraja la Kwanza.
Kituo cha Sumbawanga kitakuwa na timu za Small Kids (Rukwa), Ilonga FC (Mbeya), Mlale JKT (Ruvuma), Central Police (Dar 3), Tumbaku SC (Morogoro) na mabingwa wa Iringa.
Kituo cha Kigoma kitakuwa na timu za Shinyanga United (Shinyanga), Geita Veterans (Mwanza), Polisi SC (Mara), Kasulu United (Kigoma), Rumanyika FC (Kagera) na mabingwa wa Tabora.
Singida itakuwa na timu za Polisi SC (Arusha), Babati Mashujaa SC (Manyara), Lang’ata Bora FC (Kilimanjaro), Samaria FC (Singida) na Majengo FC (Dodoma).
Kituo cha Kibaha ni Cosmopolitan (Dar 1), Mgambo Shooting (Tanga), Mailimoja United (Pwani), Sifapolitan (Dar 2), Liwale Stars (Lindi) na mabingwa wa Mtwara.
Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana leo (Mei 15 mwaka huu) imesisita kuwa iwapo mikoa ya Tabora, Iringa na Mtwara itakuwa haijawasilisha majina ya mabingwa wao katika muda uliopangwa ligi hiyo itaendelea bila timu zao kuwemo.
Mwisho wa timu kuthibitisha kushiriki na kulipa ada ya ushiriki ya sh. 70,000 ni Mei 20 mwaka huu. Mei 28 mwaka huu ndiyo siku ya mwisho ya kurudisha fomu za usajili.Boniface Wambura
Ofisa Habari TFF

No comments:

Post a Comment