KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 19, 2011

Nembo ya Blog ya Tanzanianblogspotawards

Kutokana na maombi ya wengi ambayo tumeyapokea. Tumeongeza muda wa kupendekeza majina yatakaoshiriki katika mashindano yetu. Hivyo tarehe ya kutuma majina ya blog hizo umebadilishwa kutoka tarehe 31 May 2011 kwenda tarehe 10 June 2011.Pia sasa hivi tumeamua logo ya shindano hili ni hii hapa...Kuna nyingine tulitengeneza mwanzoni lakini hii ndio tumeichagua kwa sasa. Sasa kama ukipost habari za shindano hili tafadhali tumia picha hii.Pia kutokana na blog mbalimbali zimepost hili shindano letu na tumeona kuna maswali ambayo hayana majibu kwenye comments zao. Na sisi kwa vile hatutaweza kupitia kila blog iliyopost maelezo na kuwaelewesha watu. Hapa nitaweka majibu ya maswali baadhi nimeona yameandika najua kuna mengi lakini hatujaweza kuyaona. Ila kama una swali usisite kututumia.1. Kuna mtu amesema kuwa shindano letu haliwashirikishi watanzania wanaoishi nje ya nchi. Hiyo siyo kweli kabisa. 2. Shindano letu ni kwa blog zilizoandikwa kwa kiswahili tu. Hilo sio kweli pia3. Tunapendekeza wenyewe majina ya watu watakao shiriki katika shindano letu. Hio sio kweli kabisa. 4. Sio kila blog itakayowekwa kwenye Directory list yetu. Hilo sio kweli...Ukituletea blog yeyote iliyoandikwa na mtanzania mahali popote pale alipo ulimwenguni tutaiweka. Ili mradi hiyo blog inaweza kusomwa na mtu yeyote. Blogs ambazo hatuziweki huku ni zile ambazo waanzilishi wa blog hizo wamezifunga na wanahitaji msomaji wa blog hiyo awe mwanachama wa blog hiyo kabla hujaweza kusoma "members only blogs".


No comments:

Post a Comment