KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 26, 2011

KABURU: Hatuna mchezaji mwenye virusi vya Yanga

MAKAMU Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' amesema, ndani ya kikosi chao, hakuna wachezaji wenye 'virusi' vya Yanga.
Kaburu alisema hayo jana alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha michezo cha Radio One.
Alisema kikosi chao kinaundwa na wachezaji wengi waadilifu na kwamba, kamwe hawajawahi kugundua kuwepo kwa baadhi yaowenye mapenzi na mahasimu wao, Yanga.
"Mimi nasema wachezaji wote waliopo Simba wanaipenda timu yao kwa dhati na wapo kwa ajili ya kuitetea klabu yao na nchi kwa jumla,"alisema Kaburu.
Aliongeza kuwa, wapo baadhi ya watu, ambao pengine kwa kutofahamu, wanapoona mchezaji anacheza chini ya kiwango, wanahisi anatumiwa na wapinzani wao kuhujumu timu.
" Wachezaji ni binadamu, kuna siku wanaweza kuamka na kujisikia vibaya na wakipangwa, wanacheza chini ya kiwango na kushindwa kuonyesha uwezo wao,”alisema.
Amewataka wanachama na mashabiki wa Simba, kuwaamini wachezaji wanaosajiliwa na klabu hiyo kwa vile kamati ya usajili ipo makini katika kazi hiyo na haifanyikazi zake kwa kukurupuka.
Aliongeza kuwa, yeye na viongozi wenzake wa Simba wana imani kubwa na wachezaji wao na wanakwenda Misri wakiwa na uhakika mkubwa wa ushindi dhidi ya Wydad Casablanca ya Morocco.
Akizungumzia usajili wa wachezaji msimu ujao, kiongozi huyo alisema wapo katika mchakato wa kumpata beki namba tano, ambaye ataziba pengo la Joseph Owino.
Owino amefanyiwa upasuaji wa goti na kutakiwa kukaa nje ya dimba kwa miezi kadhaa na kusababisha timu hiyo kuwa na pengo kubwa la mlinzi wa kati katika mechi zake za mwisho za ligi kuu ya Tanzania Bara msimu uliopita.
Mbali na kusajili beki, Kaburu alisema pia kuwa, wamepanga kumnasa mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa kutoka nje ili kuziba mapengo ya Mbwana Samatta na Emmanuel Okwi.

No comments:

Post a Comment