KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, May 15, 2011

Nchimbi kukutana na wadau wa sanaa

National Arts Council BASATA 12/05/2011
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dr. Emmanuel Nchimbi (Mb), atakutana na wasanii katika ukumbi wa BASATA kuanzia tarehe 17 Mei na tarehe 18 Mei, 2011.Waziri ataongea na wasanii kwa utaratibu ufuatao:-17/05/2011 (Jumanne) Saa 4:00 asubuhi Wasanii Wote wa Sanaa za Muziki 18/05/2011 (Jumatano) Saa 4:00 asubuhi Wasanii Wote wa Sanaa za Ufundi,Filamu na MaonyeshoIzingatiwe kwamba Waziri ataongea na wasanii wa muziki wa aina zote wakiwemo wa Kizazi kipya,Bendi,Disco, Asili,Taarab na kadhalika katika siku ya kwanza.Katika siku ya pili yaani Tarehe 18/05/2011 ataongea na wasanii wa Sanaa za Filamu,Maonyesho na Ufundi pekee.Wasanii Wote mnaombwa kujitokeza kwa wingi.Lengo kuu la mikutano hii kati ya Waziri na Wasanii ni kuongelea maendeleo ya fani za sanaa.Ghonche Materego
KATIBU MTENDAJI
Mei 15, 2011

No comments:

Post a Comment