KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 12, 2011

Noorah, Tundaman watoka na vitu vipya

Noorah

Tundaman


BAADA ya ukimya wa muda mrefu, wasanii wawili nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Tundaman na Noorah wameibuka na vibao viwili vipya.
Wakati Tundaman ameibuka na kibao kinachokwenda kwa jina la ‘Lugha gongana’, Noorah ameshusha kibao kinachoitwa ‘Starehe gharama’.
Tundaman alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, amerekodi kibao chake hicho chini ya mtayarishaji maarufu wa muziki, anayejulikana kwa jina la Maneck.
Aliongeza kuwa, picha za video ya wimbo huo zimepigwa na Kampuni ya Visual Lab Next Lever.
Kwa mujibu wa Tundaman, tayari kibao hicho kimeshaanza kusikika na redioni na kuonyeshwa kwenye vituo mbalimbali vya televisheni nchini.
Naye Noorah, ambaye ni msanii wa kundi la East Zoo alisema, kibao chake hicho kipya kimetengenezwa kwenye studio za B Hits chini ya mtayarishaji mahiri wa muziki, Hermy B.
Noorah amerekodi kibao chake hicho baada ya kuwa kimya kwa zaidi ya miaka mitatu. Alisema ukimya wake huo ulitokana na uamuzi wake wa kwenda kupiga kitabu.
Kibao hicho kinasimulia maisha ya msichana mmoja, aliyejitosa kimapenzi kwa kijana wa kiume, ambaye lugha ya Kiingereza inampiga chenga.
Licha ya kibao hicho kusimulia maisha ya msichana, kimeimbwa na Noorah mwenyewe na kuwekwa vikorombwezo na Hermy B kutokana na teknolojia inayopatikana kwenye studio yake.

No comments:

Post a Comment