KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, May 15, 2011

RATIBA KOMBE LA TAIFA


Mei 15, 2011
ROBO FAINALI KILI TAIFA CUP
Hatua ya robo fainali ya Kili Taifa Cup inaanza Mei 22 mwaka huu Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Robo fainali zitachezwa mechi mbili kwa siku. Ya kwanza saa 8.00 mchana na ya pili saa 10.00 jioni.
Mei 22 mechi ya kwanza ni Singida (Kindai Shooting Stars) na Ilala. Mechi ya pili ni Mwanza (Mwanza Heroes) na Arusha (Mount Meru Warriors). Mei 23 mechi ya kwanza ni Mbeya na Ruvuma (Ruvuma Warriors) wakati ya pili ni timu ya Taifa chini ya umri wa miaka 23 (U23) na Kagera (Lweru Eagles).
Nusu fainali ya kwanza itakayohusisha washindi wa robo fainali za Mei 22 itachezwa Mei 24. Ya pili itachezwa Mei 25 wakati Mei 26 itakuwa mapumziko. Mechi ya mshindi wa tatu itakuwa Mei 27 na fainali itachezwa Mei 28.Waamuzi watakaochezesha hatua hiyo ambao wote wana beji za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ni Israel Mujuni, Judith Gamba na Oden Mbaga. Waamuzi wasaidizi ni Samwel Mpenzu, Hamis Chan’gwalu, Saada Tibabimale, Zahra Hussein, John Kanyenye na Erasmus Jesse.
Makamishna wa mechi ni Hakim Byemba na Mrisho Bukuku wakati mtathmini wa marefa (referee assessor) ni Charles Mchau. Msimamizi wa fainali hizo ni Khalifa Mgonja ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
MALALAMIKO KILI ATAIFA CUP
Kamati ya Mashindano ya TFF iliyokutana leo (Mei 15 mwaka huu) ilipitia taarifa za michuano hiyo hatua ya makundi ikiwemo malalamiko ya timu za Mara na Dodoma ambazo zililalamikia usajili wa mchezaji mmoja katika timu za Kigoma na Kagera. Kamati haikusikiliza malalamiko hayo kwa vile yaliwasilishwa nje ya muda wa pingamizi.


Boniface Wambura
Ofisa Habari TFF

No comments:

Post a Comment