KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, April 17, 2013

KEISHA AISIMULIA NDIMU



BAADA ya ukimya mrefu, msanii nyota wa kike wa muziki wa kizazi kipya, Khadija Shaaban ameibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la Ndimu.

Khadija, maarufu zaidi kwa jina la Keisha, amerekodi kibao hicho kwenye studio za AM Records chini ya prodyuza maneke.

Katika kibao hicho, Keisha amemfananisha mwanaume kuwa sawa na ndimu, ikiwemo kwenye chakula inatengeneza ladha nzuri.

Mbali na kutengeneza ladha nzuri kwenye chakula, Keisha ameimba kwenye kibao hicho akisema, hata isipokuwepo, haimaanishi kwamba haiwezekani chakula kuliwa.

Nyota huyo, ambaye alifunika vilivyo kwenye wimbo wa ‘Bado tunapanda’ wa kundi la Tip Top Connection lenye maskani yake Manzese jijini Dar alisema, mwaka jana alijifungua mtoto wa kiume.

Pamoja na kupata mtoto, Keisha alisema bado ataendelea na kazi yake ya kukonga nyoyo za mashabiki.

Keisha alijiengua katika kundi hilo mwishoni mwa mwaka jana baada ya kutokea hali ya kutokuelewana kati yake na uongozi. Kwa sasa, Keisha anapiga muziki kwa kujitegemea.

No comments:

Post a Comment