KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, April 25, 2013

RAGE ATUNISHA MISULI, APELEKA SUALA LA OKWI FIFA



MWENYEKITI wa klabu ya Simba, Ismail Aden Rage ameendelea kusisitiza msimamo wake wa kutojiuzulu uongozi wa klabu hiyo kwa tuhuma za kutafuna fedha za mauzo ya mshambuliaji Emmanuel Okwi.

Rage, ambaye ni mbunge wa Tabora Mjini (CCM) amesema, ataendelea kubaki madarakani hadi kipindi chake cha uongozi cha miaka minne kitakapomalizika mwakani.

Mwenyekiti huyo wa Simba alitoa kauli hiyo jana wakati wa kipindi cha Jambo Tanzania kilichorushwa hewani na kituo cha televisheni cha TBC 1.

Alisema watu wanaomtaka ajiuzulu, hawana uwezo wa kumng'oa kwa sababu alichaguliwa kuiongoza klabu hiyo kikatiba.

"Hawa wamedandia hoja kama vile UDA. Mimi niko Simba kwa mujibu wa katiba, hivyo siwezi kujiuzulu kwa sababu sioni kosa langu. Kama ni fedha za mchezaji (Emmanuel Okwi) hazijalipwa," alisema Rage.

Alisisitiza kuwa, Simba imemuuza Okwi kwa dola 300,000 (sh. milioni 480) kwenda klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia, lakini fedha hizo bado hazijatua mikononi mwa uongozi.

Mwenyekiti huyo alisema Simba ilimuuza nyota huyo wa zamani wa SC Villa ya Uganda kwa nia njema ya kupata fedha na pia kumfanya mchezaji huyo anufaike kutokana na kazi yake.

"Fedha za Okwi hazijafika, kama zingefika, watu wote wangejua kupitia mfumo wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), ambao mchezaji anapouzwa, mauzo yake yanaonekana, lakini kwetu bado inasomeka sifiri," alisema Rage.

Aliongeza kuwa, kwa sasa, suala la mauzo ya Okwi liko chini ya uangalizi wa Mario Demento wa FIFA, ambaye anashughulia fedha hizo ili klabu ya Simba izipate haraka iwezekanavyo.

No comments:

Post a Comment