KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, April 29, 2013

MNYAMA AUA POLISI



SIMBA jana ilijiweka kwenye nafazi nzuri ya kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa Polisi Morogoro mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo ulikuwa wa kulipiza kisasi kwa Simba kufuatia kufungwa idadi hiyo ya mabao na Polisi katika mechi ya mzunguko wa kwanza iliyochezwa mjini Morogoro.

Kutokana na ushindi huo, Simba sasa imefikisha pointi 39 kutokana na mechi 23 ilizocheza, ikiwa bado nafasi ya nne wakati Kagera Sugar niya tatu ikiwa na pointi 40.

Polisi ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 10 lililofungwa na Bantu Admini kwa shuti kali baada ya beki Miraji Juma na kipa Juma Kaseja wa Simba kuchanganyana.

Dakika tano baadaye, Haruna Chanongo aligongeana vizuri na Ramadhani Singano 'Messi', lakini shuti la Messi lilitoka nje sentimita chache.

Chanongo, ambaye alikuwa mwiba kwa mabeki wa Polisi, aliwainua vitini mashabiki wa Simba dakika ya 33 baada ya kuifungia bao la kusawazisha. Alifunga bao hilo baada ya kupokea pasi kutoka kwa Amri Kiemba. Timu hizo zilikwenda mapumziko zikiwa sare ya bao 1-1.

Mrisho Ngasa aliiongezea Simba bao la pili dakika ya 47 kwa shuti lililogonga mwamba wa juu wa goli na mpira kutinga wavuni.

No comments:

Post a Comment