KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, April 17, 2013

JUMA NATURE AFUNGUKA


BAADA ya ukimya wa muda mrefu, msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Juma Kassim 'Nature' ameamua kutoka kivingine kwa kuwashirikisha wasanii wasiokuwa na majina kurekodi nyimbo zake.

Nature alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, ameamua kushirikiana na baadhi ya wasanii wanaokubalika katika jamii ili kuzifanya nyimbo zake ziwe na mvuto zaidi.

Kwa kuanzia, Nature alisema amemshirikisha Tunda Man katika wimbo wake mpya wa Haipotei kutokana na uimbaji wake na sauti yenye mvuto.

Aliwataja wasanii wengine anaotarajia kuwashirikisha katika nyimbo zake kuwa ni pamoja na Kitale, Kingwendu, Stoppa na Dogo Lila.

Nature alisema kwa sasa hatarajii kutoa albamu kutokana na soko la muziki huo kuyumba.

Mbali na kufyatua kibao cha Haipotei, Nature pia amezindua fulana mpya zenye jina la wimbo huo.

Nature alisema mwanzo alikuwa akizigawa bure fulana hizo kwa mashabiki wake, lakini kwa sasa ameamua kuziuza.

Alisema fulana hizo zinapatikana nyumbani kwake Mbagala Zakhem na kuongeza kuwa, fulana moja inauzwa kwa sh. 16,000.

No comments:

Post a Comment