KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, April 27, 2013

YANGA BINGWA 2013/2014

HATIMAYE Yanga jana ilitawazwa kuwa mabingwa wapya wa ligi kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2012-2013 baada ya Azam kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Coastal Union katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Sare hiyo imeifanya Azam, iliyokuwa ikipambana na Yanga kuwania ubingwa, isiwe na uwezo wa kufikisha pointi 56, ambazo tayari Wana-Jangwani wameshaziweka kibindoni. Iwapo Azam itashinda mechi zake zilizosalia, itakuwa na uwezo wa kufikisha pointi 54.

Mshambuliaji Danny Lyanga ndiye aliyezima matumaini ya Azam kutwaa taji hilo baada ya kuifungia Coastal Union bao la kusawazisha dakika ya 72. Danny alifunga bao hilo dakika chache baada ya kuingia uwanjani kuchukua nafasi ya Suleiman Kassim Selembe.

Azam ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 60 lililofungwa kwa njia ya penalti na beki Aggrey Morris baada ya Gaudence Mwaikimba kuangushwa ndani ya eneo la hatari na beki Yussuf Chuma wa Coastal Union.

MABINGWA WA JUMLA LIGI KUU:
1965 : Sunderland (Dar es Salaam)
1966 : Sunderland (Dar es Salaam)
1967 : Cosmopolitans (Dar es Salaam)
1968 : Yanga
1969 : Yanga
1970 : Yanga
1971 : Yanga
1972 : Yanga
1973 : Simba
1974 : Yanga
1975 : Mseto SC (Morogoro)
1976 : Simba
1977 : Simba
1978 : Simba
1979 : Simba
1980 : Simba
1981 : Yanga
1982 : Pan African
1983 : Yanga
1984 : Simba
1985 : Yanga
1986 : Tukuyu Stars (Mbeya)
1987 : Yanga
1988 : Coastal Union (Dar es Salaam)
1989 : Yanga
1990 : Simba
1991 : Yanga
1992 : Yanga
1993 : Yanga
1994 : Simba
1995 : Simba
1996 : Yanga
1997 : Yanga
1998 : Yanga
1999 : Mtibwa Sugar (Morogoro)
2000 : Mtibwa Sugar (Morogoro)
2001 : Simba
2002 : Yanga
2003 : Simba
2004 : Simba
2005 : Yanga
2006 : Yanga
2007 : Simba (Ligi Ndogo)
2008 : Yanga
2009: Yanga
2010: Simba SC
2011: Yanga SC
2012: Simba SC
2013: Yanga SC

No comments:

Post a Comment