KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, April 17, 2013

BARTHEZ AMPIKU KASEJA KWA UBORA

KIPA Ally Mustapha 'Barthez' wa klabu ya Yanga amewapiku kwa ubora makipa Juma Kaseja wa Simba na Mwadini Ally wa Azam.

Barthez amewapiku kwa ubora makipa hao wawili wa timu ya Taifa, Taifa Stars kutokana na kufungwa mabao machache katika michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara inayoendelea.

Takwimu zinaonyesha kuwa, kabla ya mechi ya jana kati ya Yanga na Mgambo JKT iliyotarajiwa kuchezwa mjini Tanga, Barthez alikuwa amefungwa mabao 12 katika mechi 22.

Kwa mujibu wa takwimu hizo, Mwadini alikuwa akishika nafasi ya tatu kwa kufungwa mabao 19 wakati Kaseja amesharuhusu nyavu za timu yake kutikisika mara 21.

Kabla ya mechi za jana, mabao 327 yalikuwa yameshatinga wavuni, Azam ikiongoza kwa kufunga mabao 41, ikifuatiwa na Yanga iliyofunga mabao 40.

Simba ilikuwa ikishika nafasi ya tatu kwa kufunga mabao 32, ikifuatiwa na Mtibwa Sugar iliyofunga mabao 26, Kagera Sugar imefunga mabao 24, Coastal Union imefunga mabao 23 wakati JKT Oljoro na Toto African zimefunga mabao 22 kila moja.

African Lyon inaongoza kwa kufungwa mabao mengi baada ya kuruhusu nyavu zake kutikisika mabar 35, ikifuatiwa na JKT Ruvu iliyofungwa mabao 34 na Toto African iliyofungwa mabao 33.

Yanga inaongoza ligi kwa kuwa na pointi 52 (kabla ya mechi ya jana), ikifuatiwa na Azam yenye pointi 47, Kagera Sugar yenye pointi 37 na Simba yenye pointi 36.

No comments:

Post a Comment