KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, April 25, 2013

JIM IYKE, NADIA BUHARI WATOKA KWA SIRI



LAGOS, Nigeria
HATIMAYE imebainika kuwa, mcheza filamu machachari wa Nigeria, Jim Iyke ana uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji wa Ghana, Nadia Buari.

Chanzo cha habari kimedai kuwa, Jim na Nadia wamekuwa wakiufanya uhusiano wao huo kuwa siri ili kuepuka kuandamwa na vyombo vya habari.

Kwa mujibu wa chanzo hicho cha habari, Jim na Nadia wamekuwa wakikutana kwa siri na hivi karibuni walionekana wakiwa pamoja nchini Uganda.

Wacheza filamu hao pia walionekana pamoja wakati wa ndoa ya mwanamuziki 2 Face Idibia wa Nigeria iliyofanyika hivi karibuni mjini Dubai, Falme za Kiarabu.

Sehemu zingine, ambazo Jim na Nadia wamekuwa wakionekana pamoja ni Uingereza na Afrika Kusini.

"Jim Iyke amekuwa akiichukulia Ghana kama sehemu yake ya pili ya kuishi na amekuwa akisafiri mara kwa mara kwenda Accra kumuona Nadia,"kilisema chanzo cha habari.

Imeelezwa pia kuwa, safari za Nadia kwenda Lagos hazihesabiki na hivi karibuni alikwenda mapumziko nchini Marekani, ambako alionekana akiwa na Jim.

No comments:

Post a Comment