KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, April 25, 2013

HUYU NDIYE BINTI WA GENEVIEVE



LAGOS, Nigeria
KAMA kuna mcheza filamu wa Kinigeria, anayestahili kupewa tuzo kutoka na usiri, basi ni mwingine zaidi ya Genevieve Nnaji.

Genevieve, ambaye ni miongoni mwa wacheza filamu maarufu na tajiri nchini Nigeria, amekuwa akiyafanya siri kubwa maisha ya binti yake mwenye umri wa miaka 18 pamoja na baba wa mtoto huyo.

Kuna utata mkubwa kuhusu mwanaume anayedaiwa kuzaa na Genevieve na kamwe hajawahi kumtaja hadharani.

Na hii ni kutokana na mazingira, ambayo Genevieve alipata uja uzito. Inadaiwa kuwa, alipata uja uzito wa binti huyo, anayejulikana kwa jina la Chimebuka akiwa na umri wa miaka 15.

Gazeti la National Enquirer, ambalo lilikuwa la kwanza kuchapisha picha ya mtoto wa Genevieve, liliripoti hivi karibuni kuwa, mwanaume aliyezaa na mwanadada huyo anajulikana kwa jina la Acura.

Acura alilieleza gazeti hilo kwamba, baada ya kumpa uja uzito Genevieve, hakubeba jukumu la kumtunza kutokana na mazingira ya dini zao. Dini ya Genevieve (Mkatoliki) hairuhusu msichana kupata uja uzito nje ya ndoa.

Juhudi za gazeti hilo kumtafuta Genevieve ili athibitishe madai hayo, hazikuweza kufanikiwa.

Kwa sasa, Chimebuka anaishi nje ya Nigeria na hivi karibuni alikubali kupigwa picha akiwa kwenye ufukwe wa bahari, ndani ya gari na akiwa na rafiki zake hotelini.

No comments:

Post a Comment