KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 21, 2013

AZAM YAJIWEKA PABAYA, YALAZIMISHWA SARE NA WAMOROCCO


AZAM jana ilijiweka kwenye nafasi ngumu ya kusonga mbele katika
michuano ya soka ya Kombe la Shirikisho baada ya kulazimishwa
kutoka suluhu na FAR Rabat ya Morocco.

Katika mechi hiyo ya raundi ya pili iliyochezwa kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam, Azam ilipata nafasi kadhaa nzuri za kufunga
mabao, lakini ilishindwa kuzitumia vyema kutokana na washambuliaji
wake kuwa na papara ama kupiga mashuti bila malengo.

Kutokana na matokeo hayo, Azam sasa inahitaji ushindi ama sare
yoyote ya mabao ili iweze kusonga mbele wakati timu hizo
zitakaporudiana wiki mbili zijazo mjini Rabat.

Kimsingi, Azam ilicheza vizuri katika safu yake ya ulinzi na
kiungo, lakini tatizo kubwa lilikuwa katika safu yake ya
ushambuliaji, ambayo ilishindwa kucheza kwa malengo.

Kosa lingine kubwa lililofanywa na Azam katika mechi hiyo ni kujaza
wachezaji wengi wa kiungo katikati na hivyo kushindwa kujulikana ni
mchezaji yupi aliyekuwa akicheza namba 10. Pia ilimtegemea zaidi
mshambuliaji mmoja katika kufunga mabao.

Wachezaji waliocheza nafasi ya kiungo ni Humprey Mieno, Kipre
Balou, Salum Abubakar wakati Kipre Tchetche, Khamis Mcha na John
Bocco walicheza safi ya ushambuliaji.

Akizungumza baada ya mechi hiyo, Kocha Mkuu wa Azam, Stewart Hall
alisema, pamoja na kulazimishwa kutoka sare nyumbani, bado wanayo
matumaini ya kusonga mbele.

No comments:

Post a Comment