KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 21, 2013

ANNA KIBIRA MWENYEKITI MPYA CHANETA



KATIBU Mkuu wa zamani wa Chama cha Netiboli nchini (CHANETA), Anna
Kibira mwishoni mwa wiki iliyopita alichaguliwa kuwa mwenyekiti
mpya wa chama hicho.

Katika uchaguzi huo uliofanyika mkoani Dodoma, Anna aliibuka
mshindi baada ya kupata kura 61 na kumbwaga mpinzani wake, Shyrose
Banji aliyepata kura 21.

Nafasi ya makamu mwenyekiti ilichukuliwa na Zainabu Mbiro baada ya
kupata kura 57 wakati Agness Hatibu alichaguliwa kuwa mweka hazina
baada ya kupata kura 84.

Waliochaguliwa kuunda kamati ya utendaji ya chama hicho ni
Fortunata Kabeja, Asha Sapi, Judith Ilunda, Yasinta Sylvester,
Hilder Makatobe na Penina Igwe.

Akifungua mkutano mkuu wa chama hicho, Mkuu wa mkoa wa Dodoma,
Rehema Nchimbi aliitaka CHANETA kuhakikisha mchezo wa netiboli
unakuwa sehemu ya watoto wa kike.

No comments:

Post a Comment