KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 28, 2014

YANGA YATUA TANGA, KUKIPIGA NA COASTAL UNION KESHO


Na Baraka Kaziguto, Tanga

Vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara timu ya Young Africans, imewasili
salama katika jiji la Tanga majira ya saa 6 kasorobo ikitokea jijini Dar es salaam
tayari kwa kuwakabili wenyeji timu ya Coastal Union siku ya Jumatano katika Uwanja
wa Mkwakwani.

Msafara wa watu 30 ukiwa na wachezaji 20, umewasili jijini Tanga na kufikia katika
hotel ya Central City, ambayo ndio huwa wanafikia siku zote na kikosi cha kocha
mholanzi Hans Van Der Pluijm jioni kimefanya mazoezi katika viwanja vya Gymkana
eneo la Raskazone kujiandaa na mchezo huo.

Kocha Mkuu Hans sambamba na wasaidizi wake Charles Mkwasa na Juma Pondamali
wamesema wamekuja na kikosi kilichokamilika na kushirikiana kwa pamoja na benchi
la ufundi wanaamini kitaibuka na ushindi hiyo siku ya jumatano.

Kocha msaidizi wa Young Africans Charles Mkwasa amesema vijana wake wote fit
kwa sasa baada ya kupata muda mzuri wa kupumzika kufuatia safari ndefu kutoka
nchini Uturuki mwishoni mwa wiki kisha kubadirisha hali ya hewa, na kwa sasa
anasema vijana wako vizuri.

Akiongelea mchezo wa kesho Mkwasa amesema anaua Coastal Union wana timu
nzuri ambayo imekua ikitoa upinzani mkali kwa timu nyingi za Ligi Kuu lakini anaamini
katika mchezo wa kesho jinsi walivyowaandaa vijana wake watafanya vizuri na
kuwapa furaha washabiki, wapenzi na wanachama wake.

Hali ya kikosi ni nzuri hata mara baada ya mazoezi ya leo hakuna mchezaji majeruhi
hata mmoja, hivyo wachezaji wote 20 waliokuja jijini Tanga wapo tayari kwa mchezo
huo wa kesho na kazi inabakia kwa benchi la ufundi kuchagua wamtumie nani katika
mchezo huo.

Mechi itaaanza majira ya 10 kamili kwa saa za Afrika Mashariki .
Viingilio vya mchezo:
Jukwaa Kuu Tshs 10,000/=
Mzunguko Tshs 5,000/=

Kikosi kilichopo jijini Tanga ni
Makipa: Juma Kaseja, Deogratias Munish "Dida" na Ally Mustafa "Barthez"
Walinzi: Juma Abdul, Oscar Joshua, David Luhende, Mbuyu Twite, Kelvin Yondani,
Rajab Zahir na Nadir Haroub "Cannavaro"
Viungo: Haruna Niyonzima, Hamis Thabit, Nizar Khalfan na Haruna Niyonzima
Washambuliaji: Didier Kavumbagu, Jerson Tegete, Mrisho Ngasa, Saimon Msuva,
Hussein Javu na Said Bahanuzi

No comments:

Post a Comment