KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 28, 2014

YANGA YAINGIZA MIL 86/- SIMBA YAINGIZA MIL 53/-



Mechi za Ligi Kuu ya Vodacom zilizohusisha timu za Simba na Yanga na kuchezwa
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wikiendi zimeingiza jumla ya sh. 139,850,000.

Yanga iliyoibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ashanti United pambano lake
liliingiza sh. 86,035,000 kutokana na watazamaji 14,261. Mechi ya Simba ambayo
ilishinda bao 1-0 dhidi ya Rhino Rangers kutoka Tabora iliingiza sh. 53,815,00 kwa
watazamaji 9,629.

Mgawanyo kwa mechi ya Yanga ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh.
13,123,983.05, gharama za kuchapa tiketi sh. 2,910,300 wakati kila klabu ilipata sh.
20,650,211.50.

Uwanja sh. 10,500,107.54, gharama za mechi sh. 6,300,064.53, Bodi ya Ligi sh.
6,300,064.53, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 3,150,032.26 na
Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 2,450,025.09.

Mechi ya Simba mgawo ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh.
8,209,067.80, gharama za kuchapa tiketi sh. 2,910,300 wakati kila klabu ilipata sh.
12,595,211.50.

Uwanja sh. 6,404,344.83, gharama za mechi sh. 3,842,606.90, Bodi ya Ligi sh.
3,842,606.90, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,921,303.45 na
Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,494,347.13.

Vilevile tiketi zinapatikana kupitia maduka ya CRDB Fahari Huduma ambayo yapo
katika maeneo mbalimbali nchini. Watakaonunua kupitia maduka hayo watapata tiketi
na kwenda moja kwa moja uwanjani.

No comments:

Post a Comment