KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 19, 2014

SIMBA YAPIGISHWA KWATA NA MTIBWA SUGAR



BAO pekee la Masoud Ally ‘Chile’, jioni hii limeipa ushindi wa 1-0 Mtibwa Sugar ya
Morogoro dhidi ya Simba SC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa
kirafiki.
Masoud alifunga bao hilo akimalizia pasi nzuri ya kiungo wa pembeni Jamal Mnyate
dakika ya 64 ya mchezo huo mkali na wa kusisimua.
Huo ni mchezo wa pili mfululizo Simba SC kufungwa chini ya kocha mpya, Mcroatia,
Zdravko Logarusic baada ya awali kufungwa na KCC ya Uganda katika ya Kombe kla
Mapinduzi.
Awali, Logarusic aliiongoza Simba SC kushinda mechi saba mfululizo, ikiwemo ya
Nani Mtani Jembe dhidi ya wapinzani, Yanga SC mabao 3-1.
Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Yaw Berko, William Lucian ‘Gallas’/Nassor Masoud
‘Chollo’, Omar Salum/Adeyoum Saleh, Gilbert Kaze, Donald Mosoti, Awadh Juma,
Ramadhani Chombo ‘Redondo’, Edward Christopher, Betra Mombeki/Zahor Pazi, Ali
Badru na Said Ndemla.
Mtibwa Sugar; Hussein Sharrif ‘Casillas’, Said Mkopi ‘Mpiluka’, Paul Ngalema,
Salvatory Ntebe, Salum Mbonde, Shaaban Nditi, Ally Shomary, Masoud Ally ‘Chile’,
Juma Luizio, Jamal Mnyate, Ally Mohammed ‘Gaucho’/Vincent Barnabas

No comments:

Post a Comment