KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, January 20, 2014

YANGA 2 SIMURG PIK 2



Kapteni wa Young Africans Mbuyu Twite (kushoto) na kapteni wa Simurq PIK Ruslan Poladov wakibadilishna beji za timu kabla ya mchezo kuanza.



Young Africans imekamlisha ziara ya kambi yake nchini Uturuki bila ya kupoteza mchezo hata mmoja baada ya leo kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya timu ya Simurq PIK inayoshiriki Ligi Kuu nchini Azerbajain katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika jioni ya leo katika viwanja vya Side Star Hotel Complex Manavgat jijini Antalya Uturuki.

Mchezo wa leo dhidi ya Simurq PIK ulikuwa ni mchezo wa nne kwa Young Africans tangu kuwasili nchini Uturuki ambapo imeweza kushinda michezo mwili dhidi ya Ankara Sekerspor 3-0, na Altay SK 2-0 zote za Ligi Daraja la pili nchini Uturuki kabla ya kutoka sare na timu ya KS Flamurtari ya Ligi Kuu nchini Albania.

Dakika ya 13 ya mchezo mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Burundi, Didier Kavumbagu aliipatia Young Africans bao la kwanza kufuatia pasi nzuri ya mshambulaji Emmanuel Okwi na Didier kuukwamisha mpira wavuni na kumuacha mlinda mlango wa Simurq PIK Pawel Kapsa akiduwaa.

Simuriq PIK walifanya shambulizi kupitia kwa kwa kiungo wao Stephan Polyak lakini golikipa wa Young Africans Juma Kaseja alikoa hatari hiyo, huku Tagim Novruzov akishindwa kumalizia mpira uliotoka sentimeta chache langoni.

Dakika ya 30 ya mchezo Young Africans ilijipatia bao lake la pili kupitia kwa kiungo Mrisho Ngasa ambaye aliwatoka walinzi wa Simurq kufuatia migongeo mizuri katika Niyonzima, Okwi , Kavumbagu na kumkuta Ngasa ambaye aliukwamsiha mpira katika nyavu ndogo.

Mpira wa krosi uliopigwa na nahodha wa Simurq Ruslan Poladov uliwapita walinzi wa Young Africans wakishindwa kuucheza na kumkuta mlinzi wa kati Anderson Oliveira aliyepanda kusaidia mashambulizi aliyeipatia timu yake bao la kusawazisha.

Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwaza, Young Africans 2 - 1 Simurq PIK.

 Kipindi cha pili kilianza kwa Young Africans kufanya mabadiliko ambapo Nadir Haroub "Cannavaro" aliingia kuchukua nafasi ya Kelvin Yondani huku kiungo Hamis Thabit akichukua nafasi ya kiungo mkabaji Frank Domayo "Chumvi".

Dakika ya 56 ya mchezo Simuriq PIK walipata bao la pili na la kusawazisha kupitia kwa mshambulaji wao Murad Sattarli baada ya kazi nzuri iiyofanywa na kiungo wao Stephan Polyak na mpira huo kuwapita walinzi wa Young Africans na kumkuta mfungaji.

Mara baada ya bao hilo, timu zote ziliendelea kushambuliana kwa zamu lakini mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 2 - 2 Simurq PIK.

Mara baada ya mchezo wa leo kocha mkuu wa Young Africans mholanzi Hans Van Der Plyum amesema vijana wake wamecheza vizuri kwa kufuata maelekezo, ana muda wa wiki moja lakini tayari anaona mabadiliko kiuchezaji na kutegemea kufanya vizuri katika mashidano yatakayotukabili.

"Timu imecheza vizuri nawapongeza vijana kwa kujituma, hakuna lisilowezekana katika mpira, wachezaji wangu sasa hivi wanajiamini na wanajua wanatakiwa wafanye nini kwa wakati muafaka, ilikua mechi nzuri sana hata kocha wa Simurq PIK amefurahi uwezo wetu" alisema Hans.

Mara baada ya mechi ya leo timu itaendelea na mazoezi kesho asubuhi kuendelea kujiweka fit kabla ya kuanza safari ya kurejea nchini katikati ya wiki hii tayari kwa ajili ya mzunguko wa Pili wa Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya kimataifa.

Young Africans: 1.Juma Kaseja, 2.Juma Abdul, 3.Oscar Joshua, 4.Mbuyu Twite, 5.Kelvin Yondani/Nadir Haroub, 6.Frank Domayo/Hamis Thabit, 7.Mrisho Ngasa/Saimon Msuva, 8.Haruna Niyonzima, 9.Didier Kavumbagu, 10.Emmanuel Okwi, 11.David Luhende/Said Bahanuzi

Simurq PIK: 1.Pawel Kapasa, 2. Ruslan Poladov , 3.Dilaver Zrnanovich, 4.Tural Axundov, 5.Anderson De Oliveira, 6.Tagim Novruzov, 7.Nichat Kurbanov/Bashir Jamilu, 8.Patrick Osiako, 9.Salif Ballo, 10.Rashad Ayyubov, 11.Stepahn Polyak

No comments:

Post a Comment