KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 19, 2014

COASTAL YACHANUA OMAN



Na Mahmoud Zubeity, Muscat

COASTAL Union imelazimishwa sare ya bila kufungana na Seeb Club ya Oman
kwenye Uwanja wa Seeb, mjini Muscat jioni hii katika mchezo mzuri wa kirafiki.
Ikimtumia mshambuliaji aliye majaribioni kutoka Ruvu Shooting ya Tanzania, Elias
Maguri, Seeb ilionyesha upinzani mkali kwa Coastal tangu mwanzo hadi mwisho wa
mchezo.
Seeb walikuwa wakicheza kwa kupiga pasi nyingi za haraka uwanjani, wakati Coastal
ilitumia mipira mirefu na mashambulizi ya kutokea pembeni.

Mshambuliaji wa Coastal Union, Atupele Green akiwania mpira dhidi ya mabeki wa
Seeb leo

Haruna Moshi ‘Boban’ aliyeanza pamoja na Mganda Yayo Lutimba mbele waliisumbua
ngome ya Seeb na Danny Lyanga na Atuepele Green waliwasumbua mabeki wa
pembeni wa timu hiyo ya katikati ya jiji a Muscat.
Baada ya mchezo wa leo, Coastal itacheza mechi moja zaidi na timu ambayo itatajwa
baadaye, kufuatia Al Thuwaiq kugoma kucheza nao kwa madai hawakuwa na taarifa
za uhakika.
Katika mechi zake tatu za awali, Coastal ilizifunga 2-0 kila timu Nadi Oman na
Musannaa kabla ya kufungwa 1-0 na Fanja.

No comments:

Post a Comment