KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 26, 2014

SIMBA, YANGA, AZAM ZAANZA VYEMA MZUNGUKO WA PILI WA LIGI KUU



TIMU kongwe ya Simba jana iliuanza vyema mzunguko wa pili wa ligi kuu ya soka ya
Tanzania Bara baada ya kuichapa Rhino Rangers bao 1-0 katika mechi iliyopigwa
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Bao pekee na la ushindi la Simba lilifungwa na mshambuliaji machachari, Ramadhani
Singano 'Messi katika dakika ya 14.
Simba ilifanikiwa kupata mabao mengine mawili, moja katika kila kipindi, lakini
yalikataliwa na mwamuzi Andrew Shamba kwa madai kuwa yalitendeka madhambi
kabla ya mpira kujaa wavuni.
Simba ilipata nafasi nyingine nzuri ya kufunga bao kipindi cha pili baada ya
kuzawadiwa penalti, kufuatia beki mmoja wa Rhino kuunawa mpira ndani ya eneo la
hatari, lakini shuti la Messi lilimlenga kipa Charles Mpinuki wa maafande hao wa
jeshi.


Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita, mabingwa
watetezi Yanga waliichapa Ashanti mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Nayo Azam iliendelea kujichimbia nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo baada ya
kuichapa Mtibwa Sugar bao 1-0 kwenye uwanja wa Chamazi wakati Mbeya City
iliitambia Kagera Sugar ugenini baada ya kuichapa bao 1-0 kwenye Uwanja wa
Kaitaba.
Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita, Coastal
Union ilitoka sare ya bao 1-1 na JKT Oljoro kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

No comments:

Post a Comment