KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 23, 2014

SIKU ZOTE NILIKUWA WA MWISHO KULIPA ADA YA SHULE-RITHA


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu Ruth Kadiri wa Nigeria amethibitisha taarifa zilizoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari hivi karibuni kwamba, siku zote alikuwa mwanafunzi wa mwisho kulipa ada ya shule katika darasa lake wakati alipokuwa anasoka sekondari.

Binti huyo, ambaye anatoka katika familia maskini, kwa sasa ana shahada ya kwanza ya mawasiliano ya umma, aliyoipata kutoka Chuo Kikuu cha Nigeria.

"Ni kweli siku zote nilikuwa wa mwisho kulipa ada ya shule. Nakumbuka nilipokuwa kidato cha tatu, wanafunzi wenzangu wawili waliacha shule kwa sababu ya kushindwa kulipa ada," amesema mwanadada huyo msomi.

Ruth amesema kwa sasa anaye mpenzi, lakini hakuwa tayari kutaja jina lake kwa hofu ya kuandamwa na vyombo vya habari.

"Nafikiri kumpenda mtu hakuwezi kuamua furaha yako, lakini unapojipenda wewe mwenyewe kuliko unavyompenda mtu mwingine, kunakupa furaha kubwa,"amesema.

Ruth amesema kujipenda kwake binafsi ndiyo siri kubwa ya furaha yake.

"Unataka kusema kwamba kama sipo kwenye uhusiano, furaha itakuwa mbali na mimi? Hapana. Mapenzi ni kitu kizuri na chakula katika mioyo yetu, lakini nimeshafikia hatua ya kujitambua mimi ni nani,"amesema.

Alipoulizwa ni lini anatarajia kufunga ndoa, Ruth alisema: "Naomba kwa Mungu iwe hivyo kwa sababu mpenzi wangu ni mtu anayeheshimu hisia zangu, ananiunga mkono katika kazi yangu na amenionyesha mapenzi mwanana."

No comments:

Post a Comment