KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 21, 2014

BAWAZIR AIPIGA JEKI UHURU SC


Mwenyekiti wa CCM kata ya Jangwani, Mohamed Bawazir akizungumza wakati wa hafla hiyo
Mwenyekiti wa CCM kata ya Jangwani, Mohamed Bawazir (kulia) akikabidhi mpira kwa Katibu wa klabu ya michezo ya Uhuru, Rashid Zahor (kushoto), ikiwa ni sehemu ya vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh. 450,000 alivyotoa msaada kwa timu hiyo juzi katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi za Uhuru Publications Ltd, inayochapisha magazeti ya Uhuru, Mzalendo la Burudani, zilizoko barabara ya Lumumba, Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM tawi la Uhuru, Chamwingi Mpondachuma. (Picha na Yassin Kayombo).

Mwenyekiti wa CCM kata ya Jangwani, Mohamed Bawazir (kulia) akikabidhi jezi kwa Katibu wa klabu ya michezo ya Uhuru, Rashid Zahor (kushoto), ikiwa ni sehemu ya vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh. 450,000 alivyotoa msaada kwa timu hiyo juzi katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi za Uhuru Publications Ltd, inayochapisha magazeti ya Uhuru, Mzalendo la Burudani, zilizoko barabara ya Lumumba, Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM tawi la Uhuru, Chamwingi Mpondachuma
 
Mwenyekiti wa CCM kata ya Jangwani, Mohamed Bawazir (kulia) akikabidhi jezi kwa Katibu wa klabu ya michezo ya Uhuru, Rashid Zahor (kushoto), ikiwa ni sehemu ya vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh. 450,000 alivyotoa msaada kwa timu hiyo juzi katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi za Uhuru Publications Ltd, inayochapisha magazeti ya Uhuru, Mzalendo la Burudani, zilizoko barabara ya Lumumba, Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM tawi la Uhuru, Chamwingi Mpondachuma
Bawazir akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Uhuru SC na wajumbe wa kamati ya siasa na halmashauri kuu ya tawi la CCM la UPL


MWENYEKITI wa CCM kata ya Jangwani, Ilala, Dar es Salaam, Mohamed Bawazir, ametoa msaada wa vifaa vya michezo kwa timu ya soka ya Uhuru.

Bawazir alikabidhi vifaa hivyo vya michezo kwa Katibu wa Uhuru SC, Rashid Zahor, katika hafla iliyofanyika juzi kwenye ofisi za CCM za tawi la Uhuru, zilizopo barabara ya Lumumba, Dar es Salaam.

Uhuru SC, inaundwa na wafanyakazi wa Kampuni ya Uhuru Publications Ltd, inayochapisha magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani pamoja na kituo cha Redio cha Uhuru FM.

Vifaa vilivyotolewa na Bawazir kwa Uhuru SC ni seti moja ya jezi na mpira mmoja, vyote vikiwa na thamani ya sh. 450,000.

Akizungumza katika hafla hiyo, Bawazir alisema jezi hizo na mpira ni sehemu ya vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh. milioni tano, anavyotarajia kuvitoa kwa timu mbalimbali za soka za kata ya Jangwani.

Alisema ameamua kutoa vifaa hivyo kwa lengo la kutekeleza kwa vitendo ilani ya CCM na pia kuendeleza soka katika kata hiyo kwa kuzisaidia timu zinazoshiriki katika ligi za madaraja mbalimbali ili ziweze kupata mafanikio.

"Nimeamua kuanzia na timu ya Uhuru kwa sababu hapa ndiko nilikolelewa. Uhuru ni nyumbani kwangu. Nitaendelea kuisaidia timu yenu kila nitakapopata nafasi na uwezo wa kufanya hivyo,"alisema.

Mwenyekiti huyo wa CCM kata ya Jangwani pia aliahidi kutoa vifaa vya michezo kwa timu ya netiboli ya Uhuru, ambayo pamoja na ya soka, zinatarajiwa kushiriki kwenye mashindano ya kuwania Kombe la Shirika la  Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), yanayotarajiwa kuanza mwishoni mwa Machi mwaka huu.

Naye Mwenyekiti wa CCM tawi la Uhuru, Chamwingi Mpondachuma, alimshukuru Bawazir kwa msaada huo wa vifaa vya michezo na kuahidi kuutumia vyema kuwashirikisha wafanyakazi wa UPL katika michezo.

Mpondachuma alisema msaada huo umeonyesha wazi dhamira ya Bawazir katika kuendeleza michezo katika kata yake na pia kutekeleza kwa vitendo Ilani ya CCM.

Katibu wa Uhuru SC, Zahor alimuomba Bawazir, azitafutie wadhamini timu za soka na netiboli za UPL ili ziweze kucheza mechi mbalimbali za kirafiki.

No comments:

Post a Comment