KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 19, 2014

YANGA KUCHEZA MECHI YA MWISHO UTURUKI LEO



Young Africans leo jumatatu saa 8 mchana kwa saa za nchini Uturuki sawa na saa
9 kamili kwa saa za Afrika Mashariki itashuka dimbani kucheza mchezo wake wa
mwisho wa kirafiki dhidi ya timu ya Simurq PIK inayoshiriki Ligi Kuu nchini Azerbajain
katika viwanja vya Side Manavgat.

Kocha mkuu wa Young Africans mholanzi Hans Van Der Plyum amesema watautumia
mchezo huo kama sehemu ya mwisho ya maandalizi ya kujianda na Ligi Kuu ambayo
inatarajiwa kuanza mwishoni mwa wiki ijayo ambapo watoto wa jangwani watafugua
dimba dhidi ya Ashanti United uwanja wa Taifa.

Mchezo wa kesho utakua mgumu pia, kwani timu ya Simurq PIK ina wachezaji wazuri
ambao wanatoka sehemu mbali mbali dunianina ipo katika nafasi ya tano katika
msimamo wa Ligi Kuu nchini kwao, hivyo nadhani kitakua kipimo kizuri cha mwisho
kabla ya kurejea nchini Tanzania

Akiongelea kikosi chake mara baada ya mazoezi ya asubuhi, Hans amesema
anashukuru mungu maendeleo ya timu ni mazuri, mabadiliko yapo na wachezaji
wanaonekana kumuelewa hivyo anaamini kadri siku zinavyokwenda timu itakua katika
kiwango kizuri zaidi.

"Nimeshashuhudia michezo miwili mmoja tukishinda 2-0 dhidi ya timu ya Altay SK Lidi
Daraja la pili Uturuki na jana tukitoka sare ya 0-0 dhidi ya timu ya KS Flumartari ya
Ligi Kuu Albania, kwa kweli nawapongeza vijana wanaonyesha kweli wanajua wajibu
wao na kucheza kwa kufuata maelekezo ya walimu" alisema Hans.

Aidha Hans amesema ni jambo njema timu imecheza jumla ya michezo mitatu,
ikishinda miwili na kutoka sare mchezo mmoja, huku ikifunga mabao 5 na
kutokuruhusu nyavu zake kutikisika hii yote inayonyesha timu imeiva tayari kwa
mashindano yanayotukabili.

Mpaka sasa hakuna mchezaji majeruhi hata mmoja kufuatia kiungo Hassan Dilunga
kupona malaria na kuungana na wenzake katika mazoezi.

No comments:

Post a Comment