KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 28, 2014

TIKETI ZA ELEKTRONIKI ZIPO SOKONI



Mauzo ya tiketi za elektroniki kwa mechi tatu kati ya nne za Ligi Kuu ya Vodacom
(VPL) zitakazochezwa keshokutwa (Januari 27 mwaka huu) tayari yameanza, hivyo
wanatakiwa kununua mapema.

Mechi hizo ni kati ya Coastal Union na Yanga itakayofanyika Uwanja wa Mkwakwani
jijini Tanga, Kagera Sugar na Mtibwa Sugar itakayochezwa Uwanja wa Kaitaba mjini
Bukoba na ile ya Azam dhidi ya Rhino Rangers kwenye Uwanja wa Azam Complex.

Kwa washabiki wa Dar es Salaam watakaokwenda Tanga kushuhudia mechi kati ya
Coastal Union na Yanga wanashauriwa kuanza safari wakiwa na tiketi zao mikononi,
hasa kwa wale watakaonunua kupitia maduka ya Fahari Huduma.

Tiketi pia zinaweza kununuliwa kupitia mtandao wa M-Pesa kwa kupiga namba
*150*03*02#. Kwa wanaotumia CRDB simbanking wanaingia kawaida kwa *150*03.

Vilevile tunawakumbusha washabiki kuwa kwa viwanja ambavyo tayari vina mfumo
wa tiketi za elektroniki hakuna tiketi zitakazouzwa uwanjani, hivyo wanaokwenda
kwenye mechi wanatakiwa kuwa na tiketi zao mikononi.

No comments:

Post a Comment