KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, September 15, 2011

Vidume wamuibukia Funke Akindele


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa Nigeria, Funke Akindele amezua tafrani kubwa baada ya wanaume zaidi ya 119 kutoka ndani na nje ya nchi hiyo kujitokeza kutaka kumuoa.
Kujitokeza kwa vidume hao, kumekuja baada ya mwanadada huyo kuripotiwa hivi karibuni na mtandao mmoja akisema kuwa, anahitaji mwanaume bora wa kumuoa.
Tangu taarifa hizo ziliporipotiwa na mtandao huo, vidume wengi wamekuwa wakiandika ujumbe kwa njia ya barua pepe, sms na hata kupiga simu wakieleza kuwa wapo tayari kumuoa mwanadada huyo.
Baadhi ya vidume hao wamemweleza Funke kuwa, wapo tayari kufunga naye ndoa na wengine wamejipa ujiko zaidi kwa mweleza ndio chaguo lake alilopangiwa na Jalali.
Vidume hao wanatoka katika majimbo mbalimbali ya Nigeria na wengine walithubutu kufika hadi kwenye makao makuu ya mtandao uliochapisha habari za mwanadada huyo ili kupata uthibitisho.
Mtandao huo hivi karibuni ulichapisha meseji za sms kutoka kwa vidume wote waliojitokeza kutaka kumuoa mwigizaji huyo, huku meseji nyingi zaidi zikiendelea kumiminika.

No comments:

Post a Comment