KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, September 15, 2011

Kristine (Ella) ameolewa mara mbili

Christine Hermosa

Jericho



Wengi wanaulizia kuhusiana na Miguel na Ella kuwa wapenzi na kuwa na mtoto kutokana na taarifa za ndani kutoka nchini kwao Ufilipino kwamba wawili hao waliwahi kuwa wapenzi miaka ya nyuma hasa baada ya kuigiza tamthilia iliyowapa umaarufu mkubwa.


Licha ya simu nyingi kuulizia kuhusiana na mambo mbalimbali juu ya tamthilia hii, lakini wengi wanarudia kuuliza mara kwa mara swali kuhusiana na Jericho kama yu hai ama ameshafariki.


Tarifa za kuhusiana na kifo chake, ambazo zilivumishwa kuanzia mwaka 2000, lakini picha zake zinaendelea kuonekana na bendi yake ya muziki inapiga huku yeye akiimba na kuburudisha wapenzi wake katika kumbi mbalimbali hivyo jibu unalo.


Licha ya swali hilo, pia kuna swali lingine watu wakitaka kujua kuhusiana na mahusiano yake na Kristine Hermosa (Ella). Ukweli ni kwamba mwaka 2010, mwenyewe kwa mdomo wake alitamka kuwa na mpango wa kumuoa aliyekuwa mtangazaji wa Televisioni ya CNN, anayeitwa Cesca Litton huku akidai kufika hapo kwa kuwa kuna tofauti kubwa na alikowahi kupita.


Alisema kuwa wakati alipokuwa katika uhusiano na wapenzi anaodaiwa alikuwa nao kimapenzi, ambao ni Kristine Hermosa (Ella), Heart Evangelista, Gabby Conception, Lorna Tolentino na Mmalasia, Carmen Soo alijikuta akikumbwa na mambo mengi ya hapa na pale kutokana na umaarufu wa wasichana hao, lakini tangu afike kwa Cesca, amekuwa akijisikia huru zaidi na kufurahia mapenzi yake.


"Huku sifichi kitu, najisikia huru kueleza uhusiano wangu na Litton tofauti na nilipotoka kwani kulikuwa na mambo mengi yaliyokuwa yakiibuka kila siku, hivyo huku kuna tofauti kubwa na nilikotoka,'' alinukuliwa hivyo.


Jericho amezaliwa Septemba 22, 1970 katika mji wa Quezon na kuanza kazi ya uigizaji mwaka 1996, ambapo alichukuliwa kuwa mwanaume mwenye mvuto katika sanaa hiyo na kuanzia hapo alizidi kujizolea tuzo mbalimbali kwa kila tamthilia aliyokuwa akicheza.


Sasa licha ya kuigiza ni mmiliki wa bendi ya muziki aliyoipa jina la 'The Hunks', ambayo anashirikiana na wasanii Carlos Agassi, Piolo Pakual na wengineo.


Kwa upande wa Kristine Hermosa, ambaye ameigiza kama Angela (Ella) Alferos katika tamthilia hii, alizaliwa Septemba 9,1983 huko Quezon City, ambapo mji na mwenzi wa kuzaliwa unafanana na wa Jericho.


Kristine alipata bahati ya kuingia katika uigizaji baada ya mtayarishaji wa tamthilia kutoka kampuni ya picha za Televisioni ya ABS-CBN kuvutiwa naye na kumwacha dada wa Kristine, Kathleen ambaye sura yake haikumvutia mtayarishaji huyo.


Mwigizaji huyo amechanganyika kwani baba yake ni raia wa Ufilipino wakati mama yake ni raia wa Hispania. Kristine aliwahi kuolewa na Diether Ocampo na kuachana kwa madai ya wivu kwa Jericho.


Baada ya kuachana na Ocampo, Januari 12, 2011, Kristine aliolewa tena kwa ndoa na Oyo Sotto, ndoa ambayo ilisherehekewa majira ya saa tano usiku katika ukumbi wa Umbu Balai Isabel katika mji wa Talisay Batangas na sherehe hizo zilihudhuriwa na wageni 150 tu walioalikwa.


Licha ya hayo, ndoa hiyo pia iliripotiwa na kituo cha televisioni cha nchini Filipino cha SNN, ambapo sherehe za harusi hiyo zilitajwa kufadhiliwa na Rais wa Kampuni ya ABS-CBN, prodyuza pamoja na mtaalamu wa ufundi wa kampuni hiyo, ambapo dada wa Kristine, Katheleen na dada wa Oyo walikuwa wasimamizi wakuu wa harusi hiyo.

No comments:

Post a Comment