KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, September 16, 2011

SEMINA YA COM-UNITY

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira Duniani (FIFA) wameandaa semina ya siku tatu itakayofanyika Dar es Salaam kuanzia Oktoba 25-28, 2011 kwenye hoteli ya Peacock.

Semina hiyo inalenga kuwaleta pamoja wadau wote muhimu katika maendeleo ya mpira wa miguu kwa wanawake. Wadau wakuu ni Serikali, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, wadhamini na wanahabari.

Lengo kuu ni kutoa mwamko na kujenga uelewa zaidi wa mchango wa mpira wa miguu kwa wanawake katika jamii. Pia kutambua nafasi na umuhimu wa wadau mbalimbali katika maendeleo ya mpira wa miguu kwa wanawake na pia kujadili na kubaini mipango, mikakati na michango mbalimbali inayotolewa/inayoweza kutolewa na wadau hao katika kumwendeleza mtoto wa kike na ushiriki wake katika mpira wa miguu.

Semina hii inalenga kujenga stadi za mawasiliano na udhamini/masoko (marketing) ili kuliwezesha shirikisho kuzitumia na kuwavutia wadhamini na wadau wengi zaidi. Semina ya Com –Unity itatoa nafasi kwa Serikali, NGOs wadhamini na wanahabari kutoa mada mbalimbali kuhusiana na michango yao na nafasi zao katika kuendeleza mpira wa miguu kwa wanawake.

Itahitimishwa kwa Tamasha la watoto wa kike watakaocheza katika mfumo wa wachezaji watano watano Oktoba 28 mwaka huu katika viwanja vya Karume kuanzia saa tatu asubuhi. Shule zifuatazo zitashiriki;

SOS·
Ilala Boma Shule ya Msingi ·
Kurasini mahitaji maalum ·
Uhuru Mchanganyiko/Uhuru Girls·
International School of Tanganyika·
Almuntazir Girls Primary School

Mchana tunatarajia kuwa na tamasha la wazazi/akina mama kutoka timu mbalimbali zitakazoshiriki. Timu hizo zitajumuisha timu ya wanakamati wa maandalizi ya Com –Unity, viongozi wa mpira wa wanawake na wanahabari toka vyombo vyetu vya habari.

FIFA itagharamia wawezeshaji, wawakilishi wake, ukumbi na vifaa vitakavyotumika na maandalizi ya Tamasha. TFF itagharamia usafiri wa ndani, gharama za ushuru na kodi na gharama nyingine.

Kamati za Maandalizi
Kutakuwa na kamati nne za maandalizi ya Semina na Tamasha. Kamati hizo ni za uratibu wa washiriki, uandaaji na uwasilishaji wa mada, udhamini na tamasha na kamati ya habari.
Wenyeviti wa kamati hizo wataunda kamati kuu.

Kamati ya Uratibu wa Washiriki
Amina Karuma– Mwenyekiti
Michael Bundala– Katibu
Rose Kisiwa – Mjumbe

Kamati ya Udhamini na Tamasha
Rukia Mtingwa- Mwenyekiti
Jimmy Kabwe- Katibu
Devota Komba-Ikandiro – Mjumbe
Irene Mwasanga – Mjumbe

Kamati ya Habari
Joyce Mhaville/Deo Rweyunga- Mwenyekiti
Boniface Wambura– Katibu
Zena Chande – Mjumbe
Somoe Ngitu - Mjumbe

Kamati ya Uratibu wa Uandaaji wa Mada
Sunday Kayuni- Mwenyekiti
Juliana Yassoda- Katibu
Devota John – Mjumbe
Joan Minja – Mjumbe

Kamati Kuu
Lina Mhando – Mwenyekiti
Devota John Marwa – Katibu
Amina Karuma – Mjumbe
Rukia Mtingwa – Mjumbe
Joyce Mhaville/Deo Rweyunga - Mjumbe
Sunday Kayuni – Mjumbe

Mshauri na Mwezeshaji wa FIFA: Henry Tandau
Tunaomba kutoa mwito kwa wadau wa mpira wa miguu wanawake watuunge mkono. Kamati ziko tayari kupokea ushauri, misaada ya hali na mali ili kufanikisha tamasha la watoto.

Lina Mhando
Mwenyekiti
Kamati ya Semina ya Com-Unity

No comments:

Post a Comment