KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, September 15, 2011

Tonto Dikeh azusha tafrani Ghana



LAGOS, Nigeria
BAADHI ya waongozaji filamu wa Ghana wamemtaka mcheza sinema wa Kinigeria, Tonto Dikeh amwombe radhi Van Vicker, vinginevyo asahau kucheza filamu za nchi hiyo.
Kwa mujibu wa blogu moja ya mastaa wa Ghana, Van Vicker ni mmoja wa watu wanaoheshimika katika tasnia ya filamu nchini humo hivyo hawako tayari kuona akidhalilishwa kwa namna yoyote ile.
Uamuzi huo wa waongoza filamu hao umekuja baada ya kuwepo na taarifa kuwa, Tonto na Van Vicker, ambao wana uhusiano wa kimapenzi, walipigana wakiwa kwenye eneo la kutengeneza filamu.
“Hivi anaweza kumdhalilisha RMD kama vile,” alihoji mmoja wa waongoza filamu hao, ambao hakutaka jina lake litajwe.
Wameonya kuwa, watamfungia mwongoza filamu yeyote, ambaye atamshirikisha Tonto katika filamu yake. Pia wamesema wataandika barua ya malalamiko kwa Chama cha Waigizaji Filamu cha Nigeria.
Hadi sasa, Tonto hajasema lolote kuhusu onyo hilo na iwapo atakuwa tayari kumuomba radhi Van Vicker.
Mzozo kati ya Tonto na Van Vicker ulianza wakati wa mazoezi ya upigaji wa picha za filamu yao mpya, ambapo kila mmoja alikuwa akifanya mazoezi kivyake.
Baada ya muongozaji wa filamu hiyo kugundua kasoro hiyo, aliamua kuwafuata kwa lengo la kuwaweka sawa, lakini Tonto alionekana kupandwa na hasira na kuanza kusema hovyo.
Hali ilikuwa mbaya baada ya Tonto kuwasha sigara na kumpulizia moshi Van Vicker, ambaye kwa sauti ya upole, alimwomba aache kufanya hivyo ama aende kuvutia nje.
Tonto aliichukulia kauli hiyo ya Van Vicker kama kumtusi na kuanza kumtukana matusi ya nguoni. Ilibidi watayarishaji wa filamu hiyo waingilie kati kuwasuluhisha.

No comments:

Post a Comment