KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, September 15, 2011

Msondo, Sikinde zapigana madongo


BENDI kongwe za muziki wa dansi nchini, Msondo Ngoma na Mlimani Park Orchestra ‘Sikinde’ wiki hii zimeibuka na vibao vipya vyenye mwelekeo wa kupigana madongo.
Wakati Msondo Ngoma imeibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la ‘Lakuvunda halina ubani’, Sikinde wameipua kibao kinachojulikana kwa jina la ‘Bundi’.
Kibao cha Lakuvunda halina ubani kimetungwa na mwimbaji machachari wa bendi hiyo, Shabani Dede wakati kibao cha Bundi kimetungwa na Abdalla Hemba.
Akizungumza mjini Dar es Salaam juzi, Katibu wa Sikinde, Hamisi Milambo alisema kibao cha Bundi ni miongoni mwa vibao sita vitakavyokuwemo kwenye albamu mpya ya bendi hiyo.
Milambo alisema wapo katika maandalizi ya mwisho ya kurekodi kibao hicho baada ya kibao chao kilichopita cha ‘Jinamizi la talaka’ kupata mafanikio makubwa.
Kibao cha Jinamizi la talaka, kilichotungwa kwa ushirikiano wa wanamuziki wote wa Sikinde, kilirekodiwa mwezi mmoja uliopita na hivi sasa kimekuwa kikipigwa mara kwa mara kwenye vituo mbalimbali vya radio nchini.
Kufuatia kutamba kwa kibao hicho, Milambo alisema hivi sasa wapo katika hatua za mwisho za kurekodi video ya wimbo huo kwa lengo la kuwapa uhondo zaidi mashabiki. Alivitaja vibao vingine vitakavyokuwemo kwenye albamu yao mpya, watunzi wakiwa kwenye mabano kuwa ni ‘Nitalipa deni’ (wanamuziki wote), ‘Kilio cha kazi’ (Hassan Bitchuka), ‘Nisamehe’ (Hemba) na ‘Asali na shubiri’ (Shukuru Majaliwa).
Milambo alisema albamu yao mpya, itakayokuwa na vibao sita, inatarajiwa kukamilika Novemba mwaka huu kabla ya kuanza kuuzwa kwa mashabiki.
Wakati huo huo, mwimbaji mpya wa Msondo Ngoma, Dede amesema kibao chake kipya cha Lakuvunda halina ubani kimeshakamilika na kuanza kupigwa kwenye maonyesho ya bendi hiyo.
Dede alisema kibao hicho ni cha pili kwake tangu alipojiunga na bendi hiyo miezi minne iliyopita. Kibao chake cha kwanza kinajulikana kwa jina la ‘Suluhu’.
Mwimbaji huyo wa zamani wa Sikinde ametamba kuwa, kibao hicho kipya kitawadhihirishia mashabiki kwamba hana mpinzani katika utunzi na uimbaji wa nyimbo mwanana.
Dede alisema vibao alivyovitunga akiwa Msondo Ngoma havina lengo la kuwasema wanamuziki wa Sikinde kwa vile hana ugomvi nao, bali amevitunga kutokana na hisia zake.
“Sina ubaya wowote na wanamuziki wa Sikinde kwa sababu kuondoka kwangu kule kulilenga kuongeza changamoto na ushindani wa kimuziki.

No comments:

Post a Comment