KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, January 19, 2011

G-Nako aamua kutoka kivyake


MSANII George Nako wa kundi la Twenty Eleven lenye maskani yake mkoani Arusha, ameamua kurekodi singo yake inayojulikana kwa jina la ‘Oooh’.
George, ambaye pia anajulikana kwa majina ya G-Nako, The Finest of AR na Mr. Swagnificent amerekodi singo hiyo kwa kushirikiana na msanii Jade.
Msanii huyo mwenye sura na umbo lenye mvuto amesema, singo yake hiyo ni utambulisho wa albamu yake ya kwanza inayotarajiwa kutoka hivi karibuni ikiwa na nyimbo nane.
"Nakuja na albamu yangu itakayokuwa na nyimbo nane, tano nimekwishazitengeneza na nyingine tatu ziko jikoni zinapikwa, zikiwa tayari naingiza albamu sokoni," alisema.
Hata hivyo, G-Nako alisema maandalizi ya albamu yake hiyo hayawezi kuathiri kazi za kundi lake, ambalo linatesa vikali kimuziki ndani ya jiji la A-Town.
"Nipo kazini kotekote. Nikiwa na kundi langu nakamua mpaka mwisho na nikiwa solo, mwendo ni huo huo. Mashabiki wangu na wa kundi wanalijua hilo," alisema G-Nako.
Msanii huyo alisema, iwapo atatokea mtu na kumuuliza anunue albamu ipi, kati ya ile ya kwake na ya kundi iwapo zitaingizwa sokoni pamoja, alisema: " Ukimpenda G-Nako, utawapenda Nako2Nako Soldiers, hivyo hapo itabidi tu ununue albamu zote ili ufaidi," alisema.
Kwa mujibu wa G-Nako, amerekodi kibao cha Oooh katika studio za Sababisha Records chini ya watayarishaji muziki, B. Hits na Panchi Latino.

No comments:

Post a Comment