KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, January 19, 2011

Genevieve akana kuwa mja mzito

LAGOS, Nigeria
MWIGIZAJI nyota wa kike wa Nigeria, Genevieve Nnaji amekanusha madai kuwa, ana uja uzito wa mwanamuziki nguli wan chi hiyo, D’Banji.
Genevieve, ambaye amecheza filamu zaidi ya 200 za Kinigeria, alisema wiki hii kuwa, japokuwa uvumi huo ni taarifa za heri, lakini hauna ukweli wowote.
“Sitaki kumvunjia mtu heshima kwa kusema uongo, lakini ukweli ni kwamba hakuna cha kujibu kuhusu hilo,”alisema mwigizaji huyo mwenye mvuto.
Alikuwa akijibu swali aliloulizwa na mwandishi mmoja wa gazeti la The Sun la Nigeria iwapo ni kweli ana uja uzito wa mwanamuziki huyo.
“Nimesikia uzushi mwingi kuhusu mimi, lakini angalau safari hii ni habari nzuri, japokuwa hazina ukweli,”alisema.
Hata hivyo, Genevieve alikiri kuwa ni kweli ana uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki huyo machachari wa Afrika Magharibi.
Alisisitiza kuwa, iwapo habari hizo ni za kweli, hilo litabainika kadri miezi inavyosonga mbele kwa sababu mimba huwa haijifichi.

No comments:

Post a Comment