KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, July 20, 2017

NYONI, SAIDI MOHAMED WAMWAGA WINO SIMBA, KAMUSOKO AJIFUNGA MIAKA MIWILI YANGA




KLABU ya Simba imetangaza rasmi kuwasajili beki Erasto Nyoni kutoka Azam na kipa Said Mohamed kutoka Mtibwa Sugar kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu ya Tanzania Bara.

Mipango ya Simba kumsajili Nyoni imekuja huku kukiwa na taarifa kuwa, beki huyo alishafanya mazungumzo na klabu ya Yanga na kufikia makubaliano ya kusajiliwa.

Wachezaji hao wawili walioko kwenye kikosi cha timu ya Taifa, Taifa Stars, walimwaga wino Simba saa chache kabla ya timu hiyo kwenda Rwanda kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidi ya nchi hiyo keshokutwa.

Wakati huo huo, klabu ya Yanga imemsainisha mkataba wa miaka miwili kiungo wa kimataifa wa Zimbabwe, Thamani Kamusoko.

Kamusoko amekubali kumwaga wino Yanga baada ya mvutano uliodumu kwa miezi kadhaa kuhusu maslahi.

No comments:

Post a Comment