KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, July 10, 2017

SIMBA YAMSAJILI MBONDE WA MTIBWA, YANGA YAMNASA KIPA WA CAMEROON



Klabu ya Yanga imemsainisha mkataba wa miaka miwili, golikipa wa African Lyon, Youthe Rostand, ambaye ni raia wa Cameroon baada ya kufanya vizuri msimu uliopita licha ya klabu yake kushuka daraja.

Yanga imesajili Rostand huku kukiwa na tetesi kwamba, golikipa wake,
Deogratius Munishi ‘Dida’, anafanya mipango ya kujiunga na klabu ya moja ya Afrika Kusini.

Rostand amesajiliwa Yanga ili kusaidiana na Beno Kakolanya baada ya kuwepo na taarifa kuwa, akitajwa kuondoka kwenye kikosi hicho cha Jangwani na amekuwa akihusishwa kujiunga na Singida United.

Wakati huo huo, klabu ya Simba, imemsajili beki wa Mtibwa Sugar, Salim Mbonde, kwa mkataba wa miaka miwili ili kuziba pengo la Abdi Banda anayehamia Afrika Kusini.

Mbonde amesaini saa chache baada ya kuwasili Dar es Salaam, akitokea Afrika Kusini, ambako aliiongoza timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kushika nafasi ya tatu kwenye michuano ya Kombe la COSAFA.

Taarifa zimeeleza kuwa, Mbonde amesaini mkataba huo mbele ya mfadhili wa klabu hiyo, Mohammed ‘Mo’ Dewji, ambaye kwa sasa ndiye anayeihudumia timu.

No comments:

Post a Comment