KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, July 9, 2017

MBARAKA YUSSUFU ABAKI AFRIKA KUSINI, MWAKYEMBE AIMWAGIA SIFA TAIFA STARS



MSHAMBULIAJI Mbaraka Yussuf wa Taifa Stars, amebaki nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Mbaraka, mchezaji wa zamani wa Kagera Sugar, ambaye inasemekana amejiunga na Azam kwa ajili ya msimu ujao, hakuweza kumaliza michuano hiyo kutokana na kuumia.

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga, alisema juzi usiku baada ya timu hiyo kurejea kutoka Afrika Kusini kuwa, bado hawajaelewa kipi kinachomsumbua mchezaji huyo.

“Tuliyemuacha Afrika Kusini ni Mbaraka Yusuph na taarifa ya nini kinamsumbua na anarudi lini, madaktari watatuambia,” alisema Mayanga.

Wakati huo huo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, ameipongeza Taifa Stars kwa kumaliza michuano ya Kombe la COSAFA ikiwa ya tatu.

“Nchi nzima ilitamani kuwepo hapa kuwapokea, tupo hapa tunawahakikishia vijana wa Taifa Stars kuwa, kazi waliyoifanya ni nzuri,” alisema Dk. Mwakyembe.

No comments:

Post a Comment