KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, July 9, 2017

HATIMAYE ABDI BANDA APATA TIMU AFRIKA KUSINI


SAA chache ya kuwasili nchini, beki wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars Abdi Banda, akitokea Afrika Kusini, alikokuwa akishiriki katika michuano ya Kombe la COSAFA, ameweka wazi kuwa sasa ni rasmi hatoendelea kuitumikia Simba SC msimu ujao.

Banda amejiunga na klabu ya Baroka ya Afrika Kusini kwa mkataba wa miaka mitatu na amerudi Tanzania kwa ajili ya kuaga kabla ya Julai 12, mwakahuu, kurejea Afrika Kusini kuungana na timu yake hiyo mpya inayoshiriki Ligi Kuu Afrika Kusini.

“Ni ishu ambayo imekuwa rasmi kwa sasa hivi, lakini ya muda mrefu kwa hiyo nimekuja tu nyumbani mara moja kupata baraka za nyumbani, kwani nimekuja kuaga kwa viongozi wangu wa zamani wa Simba ambao nimekuwa nao muda mrefu," alisema Banda.

No comments:

Post a Comment