KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, July 20, 2017

ALLY MUSTAFA 'BARTHEZ' AMWAGA WINO SINGIDA UNITED



Golikipa wa zamani wa Dar es Salaam Young Africans, Ally Mustafa ‘Barthez’,  ametangazwa rasmi kujiunga na klabu ya Singida United, kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania.

Kipa huyo, ambaye pia amewahi kuichezea timu ya Taifa, Taifa Stars na Simba, ametia saini mkataba wa kuichezea Singida United kwa miaka miwili.

Barthez, amejiunga Singida United, ambapo atakuwa katika ‘vita’ ya namba na golikipa wa timu hiyo, Said Lubawa.

Baada ya usajili huo, Mkurugenzi wa Singida United, Festo Richard Sanga, alisema kwa sasa wamebakiwa na nafasi moja kabla ya kukamilisha usajili.

”Kwangu mimi kwanza naona hakuna utofauti kati ya timu kubwa na Singida United. Mimi naona kawaida japo kuna jina kubwa na jina dogo kwa sababu Singida United imepanda daraja msimu huu, lakini Yanga ipo Ligi Kuu muda mrefu na timu kubwa,” alisema Barthez.

No comments:

Post a Comment