KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, July 10, 2017

DK. MWAKYEMBE ASITISHA UTEUZI WA MWENYEKITI WA BMT, DIONIZ MALINZI


WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe,ametangaza kusitisha uteuzi wa Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dionis Malinzi.

Dk. Mwakyembe alitangaza uamuzi huo jana, alipokutana na kuzungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo), Dar es Salaam.

Uamuzi huo umekuja siku chache baada ya agizo la Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, kuitaka wizara hiyo kupitia upya utekelezaji wa BMT.

Kufuatia agizo hilo la Majaliwa, Waziri Mwakyembe amesitisha uteuzi huo ili kujiridhisha kuhusu utendaji wa baraza hilo.

Julai 5, mwaka huu, wakati akiahirisha kikao cha bunge mjini Dodoma,
Waziri Mkuu Majaliwa alimuagiza Waziri Mwakyembe kufanya mapitio ya uteuzi wa baraza hilo.

No comments:

Post a Comment