KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, July 23, 2017

SINGIDA UNITED YAMNYAKUA DEUS KASEKE WA YANGA




KOCHA Mkuu wa Singida United, Hans van Pluijm, ameendelea kuibomoa Yanga baada ya kumsajili winga machachari, Deus Kaseke.

Kaseke amekuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Singida United katika kipindi cha wiki moa. Wiki iliyopita, Singida United ilimsajili kipa Ally Mustapha 'Barthez' kutoka Yanga.

Mkurugenzi wa Singida United, Festo Richard Sanga, alisema jana kuwa, wamemsainisha Kaseke mkataba wa miaka miwili.

Kaseke amemaliza mkataba wake wa miaka miwili na Yanga na muda wowote kuanzia leo, atasafiri kwenda Mwanza kuungangana na timu hiyo iliyoweka.

No comments:

Post a Comment