KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, February 1, 2015

YANGA YALAZIMISHWA KUTOKA SULUHU NA NDANDA UNITED, KISIGA ABWAGA MANYANGA SIMBA


YANGA jana ilipunguzwa kasi katika michuano ya soka ya ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kulazimishwa kutoka suluhu na Ndanda United kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkali, timu zote mbili zilipata nafasi kadhaa nzuri za kufunga mabao, lakini kikwazo kikubwa kilikuwa washambuliaji wake kutokuwa makini.

Wakati huo huo, kiungo Shaaban Kisiga ‘Malone’ amejitoa katika klabu ya Simba SC kutokana na sababu ambazo bado hazijajulikana.

Kisiga alibeba vitu vyake baada ya mechi dhidi ya Mbeya City, Jumatano iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, na kuwaambia wenzake anaondoka na anazima simu zake zote ili akipigiwa asipatikane.

Katika mchezo huo, ambao Simba SC ililala 2-1, Kisiga alitokea benchi kipindi cha pili kama ilivyo ada yake kipindi hiki chini ya kocha Mserbia, Goran Kopunovic.

Siku zote Kisiga amekuwa akitokea benchi na kwenda kubadilisha mchezo, lakini Jumatano wiki hii hakuweza kuisaidia timu kuepuka kipigo cha timu ya Manispaa ya Mbeya.

Mchezaji mwingine mkongwe, Nassor Masoud ‘Chollo’ amepewa ruhusa maalum ya kwenda kutatua mataizo ya kifamilia.

Chollo ambaye siku hiyo alikosa penalti dakika ya mwisho ambayo kama angefunga Simba SC, ilipata sare, mke wake anaumwa na wana mtoto mdogo ambaye anahitaji uangalizi wa kina, wakati nyumbani hawana msaidizi.

No comments:

Post a Comment