KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 2, 2015

MECHI ZA MWISHO FDL SASA FEB 8 NA 10

 Mechi za raundi mbili za mwisho za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa makundi yote mawili zimerudishwa nyuma kutokana na maombi ya klabu hizo kupungaza gharama za kuendelea kuziweka kambini timu zao.

Hivyo, Februari 8 mwaka huu kundi A litacheza mechi zake za raundi ya 21 wakati zile za raundi 22 ambayo ndiyo ya mwisho zitafanyika Februari 13 mwaka huu. Mechi za Februari 8 ni KMC vs African Lyon, Kurugenzi vs African Sports, Majimaji vs JKT Mlale, Kimondo vs Friends Rangers, Ashanti United vs Villa Squad, Polisi Dar vs Lipuli.

Februari 13 mwaka huu ni African Lyon vs Polisi Dar, Kurugenzi vs Lipuli, Kimondo vs Majimaji, JKT Mlale vs Ashanti United, Friends Rangers vs African Sports, na Villa Squad vs KMC.

Kwa upande wa kundi B wataanza mechi za raundi 22 Februari 10 mwaka huu ili kupisha mechi za viporo za Polisi Mara zinazomalizika Februari 5 mwaka huu. Hivyo, Februari 10 mwaka huu itakuwa ni Burkina Faso vs JKT Kanembwa, Mwadui vs Polisi Tabora, Polisi Dodoma vs Green Warriors, Rhino Rangers vs JKT Oljoro, Panone vs Polisi Mara, Geita Gold vs Toto Africans.

Raundi ya 22 itachezwa Februari 15 mwaka huu kwa mechi kati ya JKT Kanembwa vs Green Warriors, Mwadui vs Burkina Faso, Polisi Tabora vs JKT Oljoro, Polisi Dodoma vs Panone, Toto Africans vs Rhino Rangers, na Geita Gold vs Polisi Mara.  

No comments:

Post a Comment