KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 2, 2015

KIPA BORA WANAWAKE AZAWADIWA 500,000/-

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya Temeke baada ya kuibuka washindi wa mashindano ya Proin Women Taifa Cup, ambayo yalichezwa katika Dimba la Azam huku Proin Promotions na Azam wakidhamini mashindano hayo.


Nahodha wa Timu ya Pwani akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni mbili ambazo ni zawadi ya mshindi wa pili katika Mashindano ya Proin Women Taifa Cup na kumalizika kwa Temeke kuwa mabingwa kwa kuifunga Pwani goli 1- 0.
Nahodha wa Timu ya Ilala ambao ni washindi wa tatu akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni moja ambayo mshindi wa tatu katika mashindano hayo ni Ilala
 Na Mwandishi Wetu
Kipa bora wa michuano ya Kombe la Taifa la Wanawake, Belina Julius wa Temeke amezawadiwa sh. 500,000 na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara.

Dk Mukangara alitoa zawadi hiyo baada ya mechi ya fainali ya michuano iliyomalizika jana kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam. Dk Mukangara alikuwa mgeni rasmi kwenye fainali hiyo.

Temeke ndiyo walioibuka mabingwa wa michuano hiyo iliyofanyika kwa mara ya kwanza nchini baada ya kuilaza Pwani bao 1-0 katika fainali iliyoonyeshwa moja kwa moja (live) na televisheni ya Azam.

Ilala ilifanikiwa kutwaa baada ya kuichapa Kigoma mabao 3-0. Bingwa amepata sh. milioni tatu, makamu bingwa sh. milioni mbili wakati mshindi wa tatu ameondoka na sh. milioni moja katika michuano hiyo iliyodhaminiwa na kampuni ya Proin.

No comments:

Post a Comment